March 7, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Rais Samia amteua Hamza Johari kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali

Na Mwandishi wetu,Timesmajira

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amemteua, Hamza S. Johari kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Dkt. Samia amemeteua Johari kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali tarehe 3 Novemba, 2025.Aidha, taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi imesema kuwa Mhe. Johari ataapishwa tarehe 5 Novemba, 2025 saa nne Asubuhi Ikulu Chamwino, Jijini Dodoma.