Na Mwandishi Wetu,Timesmajiraonline,Dar
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan, amekuwa miongoni mwa viongozi wa kitaifa walioguswa na kifo cha msanii maarufu nchini Grace Mapunda maarufu ‘Tesa’.
Kutokana na kuguswa na kifo hicho, Rais Samia alitoa salamu za rambirambi ambapo, Tesa alipoteza maisha Novemba 2 mwaka huu, wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam.
Akitoa salamu za pole kupitia ukurasa wake wa instagram, Rais Samia alisema; “Ninatoa salamu za pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na wasanii hasa waigizaji wa filamu nchini kwa kuondokewa na ndugu yetu, Grace Mapunda.
“Kwa zaidi ya miaka 20 Grace ametumia kipaji chake kutupa burudani na kuelimisha mamilioni ya Watanzania kupitia tamthilia alizoshiriki. Mwenyezi Mungu ampumzishe pema na aendelee kuijalia familia yake faraja na subra,” aliandika Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
More Stories
RPC Kuzaga ahimiza matumizi sahihi ya silaha
Dkt.bingwa wa watoto aikabidhi Hospitali ya Kanda Mbeya mashine mbili za kutoa dawa
Askari watatu wa TANAPA wafukuzwa kazi kwa tuhuma za rushwa