Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Filipe Jacinto Nyusi ameondoka nchini baada ya kumalizika kwa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kuhusu Rasilimali Watu (Africa Human Capital Heads of State Summit) uliofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 25 na 26 Julai, 2023.
Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam , Rais Nyusi amesindikizwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Stergomena Tax (Mb.), Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila na Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji, mhe. Faustine Kasike.
More Stories
Afisa Mtendaji Wazo huru achangia madawati 20 shule ya msingi Kiomboi-Bomani
Absa Dar City waunga mkono juhudi za Serikali uboreshaji Afya
Ndejembi atoa onyo kwa waajiri wasiowasilisha michango ya wafanyakazi wao NSSF