October 5, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Rais Magufuli awataka watendaji ndani ya Serikali kusimama imara

Na Mwandishi Wetu,TimesMajira,Dodoma

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli amewataka watendaji ndani ya serikali kujiamini katika nafasi zao kwa kuchapa kazi na kuhacha dhana ya kila serikali mpya inapoingia madarakani panatokea mabadiliko.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na viongozi mbalimbali katika Ikulu ya Chamwino mara baada ya kumuapisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali Profesa Adelardus Lubango Kilangi

Rais Magufuli ametoa wito huo leo Jijini Dodoma wakati wa kumuapisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali Prof. Adelardus Kilangi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Profesa Adelardus Lubango Kilangi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika hafla fupi iliyofanyika katika viwanja wa Ikulu Chamwino mkoani Dodoma

Rais Magufuli amesema kuwa mabadiliko yatakayokuwepo ni kwenye nafasi za uwaziri kwani wapo watakaorudi na wengine hawata rudi.

“Tena siku hizi chaguo ni kubwa, nina wabunge 264 kwa hiyo uchaguzi ni mkubwa Zaidi sitaki kusema uongo”, amesisitiza Rais Magufuli.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan mara baada ya hafla fupi ya Uapisho wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Profesa Adelardus Lubango Kilangi leo tarehe 09 Novemba 2020 katika Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.

Rais Magufuli amesema watendaji hao wachape kazi wasiwe na wasi wasi, hakuna mabadiliko kwani walianza wote na watamaliza wote.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan katika picha ya pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Profesa Adelardus Lubango Kilangi watatu kutoka (kulia), Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Hamis Juma wapili kutoka (kulia), Spika Job Ndugai watatu kutoka kushoto, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi wakwanza kushoto, Naibu Spika Dkt. Tulia Ackson wapili kutoka kushoto pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge wakwanza kulia mara baada ya hafla fupi ya Uapisho wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Ikulu Chamwino mkoani Dodoma

“Yani Nianze kuapisha tena wakuu wa mikoa 26 siwezi, hata kuapisha kunachosha watabaki wale wale labda watakao staafu au kuwa na utendaji mbovu”, amesema Rais Magufuli.

“Wakuu wa mikoa na wilaya naona wanakuwa na hofu na washangaa kwanini wanapata hofu maana kama mafanikio ya serikali ni pamoja na wao, kama ni ushindi wangu wa asilimia 84.4 umechangiwa na wao kwa kazi nzuri waliofanya kwa miaka mitano, wasi wasi wanini! Ameshangaa Rais Magufuli.