Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt, Samia Suluhu Hassan leo August 07, 2023 amewasili Uwanja wa Ndege wa Songwe kwaajili ya kushiriki maadhimisho ya Siku ya wakulima (Nanenane) yatakayofanyika Siku ya Kesho August 08 Mkoani Mbeya.
Baada ya kuwasili Samia amepokelewa na kusalimiana na Viongozi mbalimbali waliojitokeza Uwanjani hapo kwaajili ya kumpokea.

Maonyesho ya Siku ya Wakulima Nanenane kwa mwaka 2023 yameambatana na kauli mbiu isemayo “Vijana na Wanawake ni msingi imara wa mfumo endelevu wa chakula”.


More Stories
Mwenge wapita nyasa,wazindua mradi wa REA
Mwenge wazindua mradi wa bil.4 Nyasa
Serikali ya Samia yaleta mageuzi ya elimu Tarime vijijini