Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Katibu Mkuu Wizara ya Afya Prof. Abel Makubi ameshiriki katika Kambi ya Mabingwa katika Hospitali ya Mkoa Mwanza, Sekou Toure (15/11/2021) kwa kufanya vipimo vya kisasa vya Moyo (Trans Thoracic Echocardiography).
Prof. Makubi ni Daktari bingwa wa Moyo na damu na amebobea katika magonjwa ya Moyo kupanuka na kushindwa kufanya kazi (Heart Failure).

Prof. Makubi Pia Echo-Sonographer (mtalaamu wa kutumia mashine ya vipimo vya Moyo).
Aidha, ametoa wito kwa wakazi wa Kanda ya Ziwa kujitokeza zaidi katika huduma hiyo ya bure kutoka kwa Mabingwa wa magonjwa mbalimbali.

More Stories
Bilioni 7 kuwainua vijana 308 sekta ya uvuvi
Clara:Miaka 50 ya Sabasaba fursa mpya za Biashara na Uwekezaji
Usajili wa Laini za Simu: Jilinde Dhidi ya Kutumiwa Vibaya kwa Utambulisho Wako