Na Judith Ferdinand,Mwanza
MALI mbalimbali zikiwemo pikipiki 825 zimekamatwa katika operesheni maalum ya kudhibiti vitendo vya uhalifu ikiwemo wizi wa pikipiki katika mikoa ya Kanda ya Ziwa huku kesi 354 zikiwa zimefunguliwa.
Oparesheni hiyo ilianza rasmi Mei 4, mwaka huu kufuatia kazi iliyofanyika kwa wiki moja ya kukusanya taarifa za kiintelejensia na za kiuhalifu ambayo.
Akizungumza Jijini Mwanza jana Mkuu wa Oparesheni Maalum za Jeshi la Polisi, SACP Mihayo Msikhela, amesema operesheni hiyo imefanyika kufuatia maelekezo ya awali ya Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Simon Sirron kwa Makamanda wa Polisi wa Mikoa ya Kanda ya Ziwa katika kikao kilichofanyika Januari 22, mwaka huu mkoani Shinyanga.
Katika kikao hicho, IGP Sirro alielekeza kufanya operesheni maalumu kwa ajili ya kukabiliana na ongezeko la uhalifu wa wizi wa pikipiki katika mikoa hiyo hali ambayo inatishia amani katika maeneo hayo.
Operesheni hiyo imechukuwa takribani mwezi mmoja kuanzia Mei 4, mwaka huu na kukamilika Mei 29, mwaka huu ikihusisha mikoa nane ya Kanda ya Ziwa ambayo ni Mwanza, Geita, Shinyanga, Simiyu, Tabora, Tarime Rorya, Mara na Kagera.
Alisema katika oparesheni hiyo Mkoa wa Mwanza walikamatwa watuhumiwa 12, injini za boti 106 katika visiwa vya Juma, Gembale na zilagula vilivyopo katika wilaya ya Sengerema,mkoa wa Tabora wamekamatwa watuhumiwa halisi watatu wa mauaji.
More Stories
BAKWATA yawazawadia washindi wakuhifadhi Qur’an
Chalamila:Dar ni salama,aelezea mafanikio na mipango ya maendeleo ya Mkoa
Ulaji vyakula vya aina moja,umri vyatajwa ongozeko la matatizo ya macho Mbeya