Na Mwandishi wetu,Timesmajira
KADA wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Lameck Nyambaya amechukua fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea Jimbo la Segerea Kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM).
Nyambaya amechukua fomu mapema leo Juni 1,2025 na kukabidhiwa na Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Ilala, Sylvester Yeredi .
Nyambaya amesema ameamua kutumia haki yake ya kikatiba kwa kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea jimbo la Segerea kutokana na kuwa na uwezo, pamoja na kumsaidia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa kazi ambazo amekuwa akizifanya .
” Nimeamua kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea Jimbo la Segerea”amesema Nyambaya



More Stories
Bilioni 7 kuwainua vijana 308 sekta ya uvuvi
Clara:Miaka 50 ya Sabasaba fursa mpya za Biashara na Uwekezaji
Usajili wa Laini za Simu: Jilinde Dhidi ya Kutumiwa Vibaya kwa Utambulisho Wako