Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online
MSANII wa muziki wa Bongo fleva anayefanya vizuri hapa nchini kwa upande wa wanawake Faustina Charles maarufu ‘Nandy’, amethibitisha kutolewa barua na aliyekuwa mpenzi wake Billnass.
Akithibitisha hilo kupitia kwenye Ukurasa wake wa Instagram Nandy amesema, kwa sasa yeye ni mke mtarajiwa kwani tayari ameshatumiwa ujumbe kuwa barua ya mpenzi wake aliyepeleka kwao imepokelewa.
“Nimepokea ujumbe kuwa barua yake imepokelewa nyumbani. Hivyo kwa sasa mimi ni mke mtarajiwa (wife to be),” ameandika Nandy kupitia kwenye Ukurasa wake wa Instagram.
More Stories
Meya akabidhi Televisheni na king’amuzi Yanga
GETHSEMANE GROUP KINONDONI yaja na wimbo wa siku yetu kwaajili ya harusi
Startimes yazindua makala ya China, Africa