Na Agnes Alcardo,Timesmajira Online
WAZIRI wa Vijana, Joeli Nanauka, amewataka vijana kushiriki kwenye michezo mbalimbali ili kukuza umoja na maendeleo katika jamii pamoja na kuimarisha afya.
Nanauka ameyasema wakati wa msimu wa nne wa mbio za Korosho(Korosho Marathon)ziliyodhaminiwa na Benki ya Exim.

Nao uongozi wa Benki ya Exim, umesema, unajivunia kuwa sehemu ya msimu wa nne wa mbio hizo uliofanyika mkoani Mtwara,ikiwa ni kuunga mkono juhudi katika michezo, ustawi wa jamii na afya.
Ambapo inaamini kuwa michezo ni jukwaa muhimu la kuhamasisha maendeleo chanya, kuimarisha uhusiano wa kijamii na kujenga taifa lenye afya bora.


More Stories
Exim yatoa madawati 80 shule ya msingi
Kiongozi wa Mwenge apongeza mradi wa maji Korogwe
Jubilei ya Dhahabu ya Sabasaba yazinduliwa kwa kishindo