Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online, Arusha
MGOMBEA Ubunge Jimbo la Arusha Mjini, Mwandishi Mwandamizi wa gazeti la Majira Pamela Mollel amechukua fomu ya kuwania kiti hicho.
Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa fomu na Katibu wa Wilaya CCM Arusha, Denis Mwita katika Ofisi za Chama Cha Mapinduzi (CCM) Pamela amesema lengo kuu ni kushirikiana na wananchi wa Arusha kuleta maendeleo.
Pamela Mollel amesema atahakikisha anaisimamia ilani ya Chama Cha Mapinduzi katika utekelezaji.

More Stories
Dkt.Mabula aomba mabonde Ilemela yatumike kwa Kilimo cha umwagiliaji
Ubovu wa barabara mlima Kilimanjaro, changamoto watalii kufikia vivutio vya utalii
Rais Samia afuturisha Makao ya watoto Kikombo