BAADA ya klabu ya Simba kuwasilisha malalamiko yake kufuatia kauli ya Makamu Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Fredrick Mwakalebela kuwa wamefanya mazungumzo na mchezaji Clatous Chama, tayari Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepeleka malalamiko hayo kwenye Kamati yake ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ambacho ndicho chombo chenye mamlaka ya kusikiliza shauri hilo.
Katika malalamiko hayo, Simba wameomba ichukuliwe hatua stahiki ili kulinda kanuni zinazotawala mpira wa miguu pamoja na weledi kwani kanuni hizo zimeweka wazi kuwa kufanya mazungumzo na mchezaji aliye ndani ya mkataba ni ukiukaji wa Kanuni za usajili.
More Stories
Bahati Nasibu ya Taifa, Vodacom zashirikiana kurahisisha miamala kidijitali
Bahati Nasibu ya Taifa, Shirika la Posta washirikiana
Team nane kuchuana ” Bwigane Tv Ramadhan Street Cup”