March 7, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Msimbazi Magharibi kutumia  mobile kliniki kusikiliza kero za wananchi

Na Heri Shaaban, Timesmajira Online -Dar 

Zaidi ya wakazi 7,000, wa mtaa wa Msimbazi Magharibi Kata ya Tabata wilayani Ilala mkoani Dar-es-Salaam,kunufaika na huduma ya mobile kliniki,kufikisha na kutatulIwa kero zao bila kufika kwenye ofisi ya mtaa.

Ambapo wananchi hao watapiga simu kupitia namba maalumu,kwenye ofisi ya mtaa kisha kuwasilisha kero yake ambayo itafanyiwa kazi na Kamati husika.

Ofisa Mtendaji wa Mtaa wa Msimbazi Magharibi Kata ya Tabata Ramadhani Hamza,akizungumza na wananchi pamoja na kamati za kutatua kero za mtaa huo,wilayani Ilala mkoani Dar es Salaam,wakati wa kuzindua huduma ya mobile kliniki ya kusikiliza kero

Akizungumza wakati akizindua huduma hiyo ya mobile kliniki,Ofisa Mtendaji wa Mtaa wa Msimbazi Magharibi,Ramadhan Hamza,lengo la huduma hiyo ni kusikiliza kero za wananchi wa mtaa huo na  kutatua changamoto zinazowakabili  kwa njia hiyo ya kidigitali.

“Mtaa wangu wa Msimbazi Mangaribi una wakazi zaidi ya 7000 na vikundi vya ulinzi shirikishi viwili,tumeunda kamati ndogo ndogo kwa ajili ya kushirikiana nao,ili  tuweze kuisaidia Serikali  kutatua kero za wananchi wa mtaa huu,”amesema Hamza.

Hamza ,amesema kuna  kero zitatatuliwa na kuishia ngazi ya mtaa,na zitakazo kuwa nje ya uwezo wao  wataziwasilisha  Kata kwa ajili ya kupelekwa Halmashauri kwa utatuzi zaidi.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Msimbazi Magharibi Kata ya Tabata Wilaya ya Ilala Harun Adam akizungumza na wananchi pamoja na Kamati za kutatua kero za mtaa huo,wakati wa uzinduzi wa huduma ya mobile kliniki ya kutatua kero

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mtaa wa Msimbazi Magharibi,Harun Adam, amesema katika uzinduzi huo wa mobile kliniki wamechagua kamati kwa ajili ya kupokea na  kutatua kero.

Adam, amesema kwa sasa mtaa wa Msimbazi Magharibi vipaumbele vyao  ni kutatua kero za mazingira na  miundombinu chakavu.