April 25, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Msalaba mwekundu watoa msaada kwa waathirika wa ukame Longido

Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online, Dodoma

MWEYEKITI wa Shirika la Msalaba Mwekundu Tanzania (TRCS) mkoani Dodoma, Tryphone Mkolokoti ambaye pia ni MNEC wa TRCS ameongoza zoezi la kugawa msaada kwa waathirika wa ukame wilayani Longido,mkoani Arusha.

Utoaji wa msaada hui ni awamu ya pili kwa waathirika hao kwani mingine imetolewa mkoani Manyara katika Wilaya ya Simanjiro na Mbulu.

Akimwakilisha Rais wa TRCS, Mh. David Mwakiposa Kihenzile (MB), MNEC Mkolokoti ametoa pole kwa wananchi hao jamii ya kifugaji kwa kupoteza mifugo yao kwa ukame na amewaahidi kuendelea kuwa nao pamoja wakati wote wa maafa.

Amewaomba waendeee kuishi katika imani ya TRCS na wawe wanachama wa mfano ili kuweza kuwa karibu katika shughuli za kusaidiana pale wanapoihitaji.

Vilevile TRCS imetoa msaada wa vyakula dawa venye virutubisho muhimu kwa watoto chini ya miaka mitano kutoka jamii hiyo ambazo familia zao zimeathirika na ukame na watoto wao kupata utapiamulo ambapo jumla ya kaya 150 zimepata vyakula hivyo.

Ndg. Tryphone Mkolokoti(TRCS-MNEC) akikabidhi pesa kwa mmoja wa waathirika wa ukame katika kijiji cha Lesing’ita wilaya ya Longido, mkoani Arusha Mradi huo unaofadhiliwa na IFRC