Na Mwandishi Wetu. Timesmajira
Timu ya Taifa ya Morocco, imekuwa nchi ya kwanza kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) za 2023, zitakazofanyika nchini Ivory Cost mwaka huu.
Inchi hiyo ilikata tiketi ya kucheza michuano hiyo jana baada ya Afrika Kusini na Liberia kupata sare ya magoli 2-2.
Morocco inaongoza Kundi K, ikiwa na alama sita baada ya kushinda mechi mbili dhidi ya Liberia na Afrika Kusini.
Zimbabwe, ambayo awali ilipangwa Kundi K, iliondolewa na FIFA kucheza mechi za kufuzu AFCON kutokana na serikali ya Zimbabwe kuingilia masuala ya ligi ya soka ya nchi hiyo.
More Stories
Bahati Nasibu ya Taifa, Selcom zashirikiana ununuzi wa tiketi
Bahati Nasibu ya Taifa, Vodacom zashirikiana kurahisisha miamala kidijitali
Bahati Nasibu ya Taifa, Shirika la Posta washirikiana