Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Aloyce Nzuki amemkabidhi rasmi Dkt. Robert Fyumagwa majukumu ya kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania- TAWIRI.
Dkt. Robert Fyumagwa anatekeleza majukumu ya Taasisi hiyo kufuatia aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori-TAWIRI, Dkt.Simon Mduma kustaafu kwa mujibu wa sheria.
Kupitia hatua hiyo tayari Dkt.Fyumagwa ameanza rasmi kutekeleza majukumu ya Taasisi hiyo kuanzia tarehe 17 Agosti, 2020.
Akizungumza Jijini Arusha katika Kikao na Menejimenti ya TAWIRI, Dkt. Nzuki amewataka watumishi hao kumpa ushirikiano Dkt. Fyumagwa katika kutekeleza majukumu yake ikiwa pamoja na kuimarisha shughuli za utafiti wa Wanyamapori pamoja na kuendeleza sekta ya wanyamapori nchini.
More Stories
Gharama Kubwa za Tiba Magonjwa Makubwa Zatajwa Bungeni
CCM yajipanga kwa Uchaguzi Mkuu 2025:Rais Samia atoa maelekezo ya kimkakati
CCM Yatangaza Vipaumbele Tisa vya Ilani ya Uchaguzi 2025–2030