Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Aloyce Nzuki amemkabidhi rasmi Dkt. Robert Fyumagwa majukumu ya kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania- TAWIRI.
Dkt. Robert Fyumagwa anatekeleza majukumu ya Taasisi hiyo kufuatia aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori-TAWIRI, Dkt.Simon Mduma kustaafu kwa mujibu wa sheria.
Kupitia hatua hiyo tayari Dkt.Fyumagwa ameanza rasmi kutekeleza majukumu ya Taasisi hiyo kuanzia tarehe 17 Agosti, 2020.
Akizungumza Jijini Arusha katika Kikao na Menejimenti ya TAWIRI, Dkt. Nzuki amewataka watumishi hao kumpa ushirikiano Dkt. Fyumagwa katika kutekeleza majukumu yake ikiwa pamoja na kuimarisha shughuli za utafiti wa Wanyamapori pamoja na kuendeleza sekta ya wanyamapori nchini.
More Stories
Serikali ,Washirika wa Maendeleo waweka mkakati utekelezaji Dira ya 2050
Benki ya Exim yazindua suluhisho la malipo ya kisasa kwenye Z- Summit 2025
DCEA yateketeza zaidi ya ekari 300 za bangi