Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online, Dar es Salaam
MGOMBEA Ubunge wa Mkoa wa Dar es salaam Viti Maalumu kupitia Chama Cha Mapinduzi Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Scholastica Mazula ambaye ni Mhariri Efm Radio na TV Eamechukua fomu ya kuwania kiti hicho leo.
Akizungumza baada ya kukabidhiwa fomu na Katibu wa UWT Mkoa wa Dar es salaam Grace Gama katika Ofisi za Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mazula amesema lengo kuu ni kushirikiana na kina mama katika kumsaidia Rais Dkt John Magufuli kuleta maendeleo nchini.
Scholastica Mazula amesema atahakikisha atashirikiana na Wana-CCM kusimamia ilani ya Chama Cha Mapinduzi katika utekelezaji.
More Stories
Wanachi wahimizwa kusajili biashara,majina ya kampuni BRELA
Manispaa ya Shinyanga yaandikisha wanafunzi wa darasa la kwanza kwa 99%
Wananchi wapongeza huduma ya kliniki ya Sheria bila malipo