Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online, Dar es Salaam
MGOMBEA Ubunge wa Mkoa wa Dar es salaam Viti Maalumu kupitia Chama Cha Mapinduzi Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Scholastica Mazula ambaye ni Mhariri Efm Radio na TV Eamechukua fomu ya kuwania kiti hicho leo.
Akizungumza baada ya kukabidhiwa fomu na Katibu wa UWT Mkoa wa Dar es salaam Grace Gama katika Ofisi za Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mazula amesema lengo kuu ni kushirikiana na kina mama katika kumsaidia Rais Dkt John Magufuli kuleta maendeleo nchini.
Scholastica Mazula amesema atahakikisha atashirikiana na Wana-CCM kusimamia ilani ya Chama Cha Mapinduzi katika utekelezaji.
More Stories
Dkt.Mabula aomba mabonde Ilemela yatumike kwa Kilimo cha umwagiliaji
Ubovu wa barabara mlima Kilimanjaro, changamoto watalii kufikia vivutio vya utalii
Rais Samia afuturisha Makao ya watoto Kikombo