March 7, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Mgombea Ubunge Ilemela kupitia CHAUMMA ataja vipaumbele vyake 

Judith Ferdinand, Timesmajira Online-Mwanza 

Mgombea Ubunge wa  Jimbo la llemela kupitia  chama cha CHAUMMA,Veronica Mgeta,ametaja vipaumbele saba ambavyo atavitekeleza endapo atapata ridhaa ya kuwa Mbunge wa Jimbo hilo katika uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 29,2025.

Veronica, amesema kipaumbele Cha kwanza ni afya ambapo atahakikisha jimboni humo kunakuwa na wauguzi WA kutosha,dawa na vifaa tiba muhimu.

Amesema kipaumbele cha pili ni elimu,ambapo akifanikiwa kuwa Mbunge, atahakikisha michango yote midogo midogo inaondolewa ili kurahisisha kila mtoto anapata elimu bora.

Pia amesema, kipaumbele chake cha tatu ni bodaboda na bajaji,ambapo atahakikisha wanakuwa na maeneo salama la kufanyia kazi bila kubuguziwa pamoja na kujenga chuo cha mafunzo na uendeshaji wa bodaboda na bajaji.

Aidha kipaumbele kingine ni machinga,ambapo atahakikisha wanatengewa maeneo yenye kufikiwa na watu  na siyo kuwapeleka mahali ambako hakuna biashara pamoja na kuwawezesha kupata mikopo kwa ajili ya mitaji.

Kipaumbele kingine ni sekta ya uvuvi bapo atahakikisha anatetea haki za wavuvi ili wafanye kazi zao kwa usawa bila kubuguziwa.

Mbali na hayo pia kipaumbele kingine ni maji ambapo akifanikiwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Ilemela,ata akikisja maeneo yote ya jimboni humo  yanapata maji safi na salama.

Huku kipaumbele cha saba ni sekta ya ardhi,ambapo atatatua migogoro yote ya ardhi na kusimamia ulipwaji wa  fidia wa haki.