October 6, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM, Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino kwa ajili ya hafla ya chakula cha mchana iliyowandalia Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM. PICHA ZOTE NA IKULU

Matukio mbalimbali katika ghafla ya chakula cha mchana Ikulu ya Chamwino Dodoma leo [PICHANI]

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM, Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akicheza mziki uliokuwa ukipigwa na Msanii Hamza Kalala na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa pamoja na Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Bashiru Ally Kakurwa katika hafla hiyo ya Chakula cha Mchana kwa Wajumbe wa Mkutano Mkuu.
Baadhi ya Mawaziri wakicheza nyimbo zilizokuwa zikitumbuizwa katika hafla maalumu ya Chakula cha Mchana iliyoandaliwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa ajili ya Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM katika Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Baadhi ya Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM pamoja na viongozi wengine wakiweka zege kama kumbukumbu katika ujenzi wa Ofisi mpya za Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Viongozi Wastaafu wa Chama cha Mapinduzi CCM pamoja na Wajumbe wengine wa Mkutano Mkuu wakicheza mziki katika hafla ya Chakula cha Mchana kwa Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM iliyoandaliwa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM, Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Wasanii wa Kizazi kipya Harmonize, Ali Kiba na Diamond wakiwa wameketi pamoja katika hafla ya chakula hicho cha mchana kwa ajili ya Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM.