June 10, 2025

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Matiko atangaza nia ya kugombea Ubunge Kivule

Na Agnes Alcardo, Timesmajira Online 

Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Mkoa wa Mara, Faustine Matiko, ameweka wazi nia ya kuwania Ubunge katika jimbo jipya la Kivule jijini Dar es Salaam, katika uchaguzi mkuu,unaotarajia kufanyika   mwaka huu.

Matiko ambaye ni mfugaji wa kuku, amewahi kugombea Ubunge Jimbo la  Musoma mkoani Mara mwaka 2020.

Akizungumza na waandishi  wa habari jijini Dar- es-Salaam,Matokeo,ametaja  vipaumbele vyake endapo atachaguliwa  kuwa Mbunge wa Jimbo hilo,ni pamoja na kuanzisha soko kuu la uzalishaji na usambazaji wa mayai ndani na nje ya nchi litakalogharimu zaidi ya bilioni 1.

Amesema,Kivule ni moja ya eneo ambalo linazalisha mayai kwa kiwango kikubwa,hivyo amechukulia kama fursa,hivyo alipata Ubunge  ataanza  ujenzi wa soko hilo ndani ya siku 100.

“Nitakapochaguliwa moja ya kipaumbele changu kama Mbunge wa Kivule ni kuanzisha soko kuu ambalo litasaidia hata wafanyabiashara kusafirisha kwa urahisi na usalama zaidi mayai,”amesema Matiko.

Pia ameahidi, kushirikiana na viongozi wa Manispaa ya Ilala  kuweka mipango thabiti ya ujengaji wa soko hilo ambalo litaweza kuwa mkombozi kwa wakazi wa Kivule pamoja na kuongeza uchumi wa taifa.

Hata hivyo ametaja kipaumbele  kingine ni kuhamasisha wanakivule kuendelea  kutumia majiko ya gesi kwa ajili ya kuimarisha matumizi ya  nishati safi  ya kupikia pamoja na uboreshwaji wa miundombinu ya barabara.