Na Mwandishi wetu, Timesmajira
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhandisi Hamad Yusuf Masauni kwa mujibu wa Kifungu Na.19 (2) (C) cha Sheria ya Usimamizi Mazingira Na. 20 ya Mwaka 2004,amefanya uteuzi wa Wajumbe wa Bodi ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC).
Taarifa iliyotolewa leo na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,Ofisi ya Makamu wa Rais, Sarah Msika amewataja wajumbe hao ni pamoja na Dkt. Abubakar Rajab,Prof.Hamisi Malebo,Prof. Theobald Theodory,Mhandisi Bashir Mrindoko na Said Habibu Tunda.
Wengine ni Alex Mgongolwa,Rabia Hamid na Mhandisi Kemilembe Mutasa ambapo uteuzi wa wajumbe hawa umeanza April 9 , 2025 na utadumu kwa muda wa miaka mitatu.
Uteuzi huu umekuja kufuatia uteuzi uliofanywa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan wa kumteua Mhandisi Mwanasha Rajab Tumbo kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),
More Stories
Mwanasheria Mkuu wa Serikali ,awafunda mawakili wa serikali
TMA yawataka wananchi kuzifanyia kazi taarifa inazotoa
TPDC, ZPDC zaendelea kushirikiana uendelezaji sekta ya gesi nchini