Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mheshimiwa Othman Masoud Othman, jioni ya leo Disemba 23, 2024, amewasili Kisiwani Pemba kwaajili ya Ziara Maalum, inayojumuisha Shughuli za Serikali, Chama na jamii.

Katika Uwanja wa Ndege wa Pemba, Mheshimiwa Othman amepokelewa na Viongozi mbali mbali wa Serikali, Chama, na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama, wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba, Ndugu Rashid Hadid, pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Chake Chake, Bi. Mgeni Khatib Yahya.



More Stories
Silinde azindua baraza la sita la Wafanyakazi Tume ya Taifa ya Umwagiliaji
NMB ilivyosaidia Serikali kukusanya zaidi ya Sh trilioni 9.8
Serikali yaongeza nguvu kwa wachimbaji wadogo,yasisitiza usalama Migodini