Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mheshimiwa Othman Masoud Othman, jioni ya leo Disemba 23, 2024, amewasili Kisiwani Pemba kwaajili ya Ziara Maalum, inayojumuisha Shughuli za Serikali, Chama na jamii.

Katika Uwanja wa Ndege wa Pemba, Mheshimiwa Othman amepokelewa na Viongozi mbali mbali wa Serikali, Chama, na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama, wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba, Ndugu Rashid Hadid, pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Chake Chake, Bi. Mgeni Khatib Yahya.



More Stories
TANESCO yabaini matukio ya Wizi wa Umeme Kinondoni
DCEA yazindua klabu kupinga dawa za kulevya vyuoni
Serikali yaimarisha uhimilivu bei za mafuta nchini