Na Mwandishi Wetu,Timesmajiraonline,Zanzibar
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Othman Masoud Othman, Leo Jumapili Oktoba 8, 2023 amefika Langoni- Maungani, Wilaya ya Magharibi B Unguja, kwaajili ya Kuwafariji na Kutoa Mkono wa Pole kwa Wanafamilia wa Mzee Ismail Sharif, Kaka wa Marehemu Maalim Seif Sharif Hamad.

Hatua hiyo imekuja kufuatia Kifo cha Hasnuu Ismail Sharif (68), aliyefariki-dunia Usiku wa Kuamkia Jumamosi ya jana, hapo Nyumbani kwao Langoni-Maungani, baada ya kuugua kwa Majuma kadhaa.



Marehemu Hasnuu ambaye amewacha Mke na Watoto Watatu (3), pia amezikwa jana katika Makaburi ya hapo-hapo Langoni-Maungani, kisiwani Unguja.


More Stories
Chalamila:Dar ni salama,aelezea mafanikio na mipango ya maendeleo ya Mkoa
Ulaji vyakula vya aina moja,umri vyatajwa ongozeko la matatizo ya macho Mbeya
Kenya,Uganda zaanzisha mradi wa uendelezaji rasilimali za maji Angololo