Na Mwandishi wetu, timesmajira
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Othman Masoud Othman, amekamilisha ziara Maalum ya kuwatembelea na kuwajulia-hali, Wagonjwa na Wazee mbali mbali wasiojiweza na pia kuwapa mkono wa pole wafiwa wa maeneo mbali mbali ndani ya Mikoa 11 ya kichama katika visiwa vya Unguja na Pemba.

Othman ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha ACT Wazalendo, alianza ziara hio Machi 19, mwaka huu katika Mkoa wa kusini Unguja na kumaliza leo katika Mkoa wa kichama wa Magharib B.

Ziara hiyo iliyoasisiwa na mtangulizi wake Marehemu Maalim Seif Sharif Hamad, imewajumuisha pia Viongozi mbali mbali wa Chama na Serikali, waliombatana na Othman, wakiongozwa na Katibu wa Idara ya Habari na Uenzezi wa ACT Wazalendo, Salim Biman.



More Stories
Huduma Hospitali ya Benjamin Mkapa zinashawishi kuwa ya Taifa
Mchango wa sekta ya madini kwenye pato la Taifa waongezeka hadi asilimia 9.0
Wizara ya Nishati yajivunia jitihada katika kulinda haki, usawa na kuwawezesha wanawake