Waziri Mkuu wa Somalia, Mohamed Hussein Roble amesema amesikitishwa na ghasia za usiku wa Jumapili iliyopita katika mji mkuu wa Mogadishu kati ya vyombo vya usalama vya serikali na vikosi vya upinzani.
Roble amesema,mazungumzo na kuelewana ndio njia pekee za kutatua mkwamo wao ambao umeendelea kuletataharuki kwa muda mrefu nchini humo.
Mapigano yaliripotiwa nyumbani kwa kiongozi wa chama cha upinzani cha Wadajir, Abdulrahman Abdishakur nanyumbani kwa Rais wa zamani, Hassan Sheikh Mohamud.
Rais huyo wa zamani ni miongoni mwa wale wanaopinga kuongezwa kwa muda wa Rais Mohamed Abdullahi Mohamed (Farmajo).
More Stories
CCM yatuma salam za pole kifo cha Baba Mtakatifu Francisko
Rais Samia aomboleza kifo cha Papa Francisko
Papa Francis afariki Jumatatu ya Pasaka akiwa na miaka 88