Na David John,Timesmajira,Online
HALMASHAURI ya Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani imeweka wazi baada ya kufanikiwa kwa tamasha la Kisarawe Ushoroba Festival mwaka 2021, imesema kwamba Kisarawe Ushoroba Festival 2022 litafanyika ndani ya wilaya hiyo na wadau wameridhia kwa kauli moja.
Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Jocate Mwegelo ameweka wazi wilaya yao imejipanga kuendelea na Kisarawe Ushoroba Festival na kwa mikakati iliyopo wana uhakika mwaka 2022 kutakuwa na mambo mengi zaidi ukilinganisha na Kisarawe Ushoroba Festival 2021.
Aidha ameanza kukaribisha wadau na kuwashukuru WWF Tanzania na Vodacom Tanzania Foundation ambao wameahidi kuendelea kudhamini tamasha hilo.
More Stories
Waislamu Mwanza wapokea Ramadhani kwa maandamano ya kidini
Kamati ya kudumu ya Bunge ya utawala,katiba na sheria yaridhishwa ujenzi soko Kariakoo
TRA Tanga yakusanya bil.178.3 kwa miezi sita