Na Mwandishi wetu,Timesmajira
SERIKALI imekemea Watanzania wanao kwenda kufanya kazi nje ya nchi bila kufuata utaratibu uliowekwa kwa mujibu wa sheria kwa kuwa inasababisha kutojulikana walipo na shughuli wanazozifanya.
Hayo yamebainishwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Ridhiwani Kikwete wakati wa uzinduzi wa utekelezaji wa makubaliano ya kuwezesha na kuratibu ajira za Watanzania nchini Saudi Arabia uliyofanyika jana Januari 27. 2024 nchini huko.

Waziri amesema uhusiano mzuri uliopo baina ya Tanzania na Saudi Arabia hauruhusu wafanyakazi kufanya kazi au kusafiri bila kufuata utaratibu, hivyo kila Mtanzania anayehitaji kufanya kazi nje ya nchi apitie kwa mawakala wanatambulika baina ya nchi hizo mbili.

Kikwete amesema miongoni mwa makubaliano yaliyofikiwa ni pamoja na kuweka utaratibu mzuri wa Watanzania kusafiri kwenda nchini Saudi Arabia, upimaji wa afya, kupata kazi zenye staha na mshahara mzuri ambao utawasaidia kujikwamua kiuchumi.
More Stories
Benki ya NMB yatenga Bil. 100/-za nishati safi kwa wajasiriamali
Bussungu,Khatibu kupeperusha bendera ya ADA-TADEA uchaguzi Mkuu
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Johari ameungana na Viongozi mbalimbali nchini kushiriki kuaga na kutoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais Hayati Cleopa Msuya