Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Francis Michael amewataka watumishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii wafanye kazi kwa bidii huku akisisitiza kuwa yeye kama kiongozi wao ataendelea kuwapa ushirikiano mkubwa katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Ameyasema hayo leo jijini Dodoma mara baada ya kuwatembelea watumishi hao katika Ofisi za Wizara ya Maliasili na Utalii zilizoko katika Chuo Kikuu cha Dodoma na kuwahakikishia kuendelea kuwapa ushirikiano mkubwa ili waweze kutimiza majukumu yao ya kila siku.

More Stories
Bilioni 7 kuwainua vijana 308 sekta ya uvuvi
Clara:Miaka 50 ya Sabasaba fursa mpya za Biashara na Uwekezaji
Usajili wa Laini za Simu: Jilinde Dhidi ya Kutumiwa Vibaya kwa Utambulisho Wako