Na Mwandishi Wetu,Timesmajiraonline
NAIBU Waziri wa Nishati Judith Kapinga ameshiriki Jukwa la Mawaziri (Ministerial Symposium)nchini Afrika Kusini ikiwa ni sehemu Kongamano la Wiki ya Mafuta Afrika (Afrika Oil Week) linalofanyika Jijini Cape Town.
Lengo la jukwaa hilo ni kutangaza fursa za uwekezaji kwenye Mafuta, Gesi Asilia na Nishati Mbadala
Jukwaa hilo pia limehudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Dkt. James Mataragio, Kamishina wa Petroli na Gesi Goodluck Shirima na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli ( PURA), Mha. Charles Sangweni.
Maudhui ya Kongamano hilo ni pamoja na kutangaza fursa za uwekezaji katika miradi ya Mafuta, Gesi Asilia na Nishati Mbadala katika Bara la Afrika.
Kongamano hilo litamalizika tarehe 10, Oktoba, 2024 nchini humo.
More Stories
Kamati ya Bunge yajionea namna WMA inavyosimamia sekta ya mafuta bandarini
Serikali yaagizwa kudhibiti wanyama wakali Kisesa
Ubalozi wa China, Kampuni ya Oryx wakabidhi mitungi 8,000 ikiwa na majiko