Na Mwandishi Wetu,Timesmajiraonline
NAIBU Waziri wa Nishati Judith Kapinga ameshiriki Jukwa la Mawaziri (Ministerial Symposium)nchini Afrika Kusini ikiwa ni sehemu Kongamano la Wiki ya Mafuta Afrika (Afrika Oil Week) linalofanyika Jijini Cape Town.
Lengo la jukwaa hilo ni kutangaza fursa za uwekezaji kwenye Mafuta, Gesi Asilia na Nishati Mbadala
Jukwaa hilo pia limehudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Dkt. James Mataragio, Kamishina wa Petroli na Gesi Goodluck Shirima na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli ( PURA), Mha. Charles Sangweni.
Maudhui ya Kongamano hilo ni pamoja na kutangaza fursa za uwekezaji katika miradi ya Mafuta, Gesi Asilia na Nishati Mbadala katika Bara la Afrika.
Kongamano hilo litamalizika tarehe 10, Oktoba, 2024 nchini humo.




More Stories
Kamati ya kudumu ya Bunge ya utawala,katiba na sheria yaridhishwa ujenzi soko Kariakoo
TRA Tanga yakusanya bil.178.3 kwa miezi sita
Wataalam Sekta ya utalii watakiwa kufanya kazi kwa uadilifu,kujituma na kuwa wabunifu