
Na Mwandishi wetu, Timesmajira Online DSM
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam limetahadharisha wale wanaofikiria kufanya uhalifu siku ya Sikuu ya Pasaka waache mara Moja watashughulikiwa ipasavyo kwani Jeshi liko Imara kuhakikisha hali ya Usalama inakuwa shwari
Akizungumza na Waandishi wa habari Jijini Dar es salaam Kamanda wa Kanda Maalumu wa Dar es salaam SACP Jumanne Muliro amesema Polisi hawatasita Kufuatilia watu watakaotaka kupanga njama za kufanya uhalifu hawatalala kwani kila sikukuu kumekuwa na baadhi yao kutumia siku hivyo hivyo Jeshi litaendelea kufanya doria kila mahali.
Hata hivyo amewaomba Wazazi,Walezi siku ya sikukuu kuwa karibu na Watoto katika siku hiyo kwani kunakuwa na kupotea kwa watoto hivyo amewasihi ni bora wasiwaruhusu kwenda kwenye kumbi za starehe wakiwa wenyewe bora wawazuie
Aidha hali ya Usalama katika Kanda ya Dar es salaam ni shwari ikilinganishwa na miaka ya nyuma kulikuwa na matukio mbalimbali ikiwemo mtu kuprwa fedha akitokea benki na hawakamatwi wahalifu lakini saa hivi Jeshi halina budi kupongezwa kwa operesheni Kali inayofanyika kila siku chini ya Kamanda SAP Jumanne Muliro
More Stories
Wataalamu wa ujenzi mfumo wa NeST wanolewa usalama wa mifumo
Mkurugenzi Rapha Group aeleza fursa mashindano Tulia Marathoni
Prof.Muhongo amshukuru Rais Samia kwa fedha nyingi miradi ya elimu Musoma Vijijini