April 23, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Jela miezi 6 kwa uzushi wa kuibiwa nyeti

Na Israel Mwaisaka, Sumbawanga

‎Mahakama ya mwanzo Ilemba Wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa imewahukumu kifungo Cha miezi 6 vijana 7 kati ya 8 waliofikishwa katika mahakama hiyo kwa kosa la uzushi wa kuibiwa nyeti wakati siyo kweli.

‎Watuhumiwa hao  walifikishwa katika mahakama hiyo baada ya kumzushia Masanja Joseph Sen  (34) mkazi wa Kijiji Cha Ilemba kuwa amewaibia nyeti ambapo walimvamia kumpiga na kumsababishia maumivu makali.

‎Mahakama hiyo chini ya Hakimu Rajabu Ukwaju iliwakuta na hatia watuhimiwa 7 kati ya 8 na kuwapa adhabu hiyo ya kifungo Cha miezi 6 jela na kulazimika kumlipa fidia ya Tshs,100,000 Kila mmoja kutokana na maumivu aliyoyapata.

‎Sambamba na hilo jeshi la Polisi mkoani Rukwa linamshikilia Bosco John Fatachi (38) mkazi wa Kijiji Cha Kambo wilayani Kalambo kwa kosa la kumshambulia mtoto wa umri wa miaka 8 akimtuhumu kumuibia Pipi yenye thamani ya Tshs,200 dukani kwake.

‎Hakimu huyo amedai kuwa ametoa adhabu hiyo ili iwe ni fundisho kwa Watu wengine Wenye tabia za uzushi kama huo.

‎Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kamanda wa Polisi mkoani Rukwa Shadrack Masija ni kuwa mtuhumiwa huyo baada ya kutenda kosa hilo alitoroka na jeshi hilo liliendelea kumtafuta hadi walipomkamata.

‎Amesema kuwa kwa Sasa wanaendelea na uchunguzi na kuwa ukikamilika watamfikisha mahakamani kujibu tuhuma hizo zinazomkabili.