Na Mwandishi Wetu,TimesMajira Online
MSANII mwenye vituko vingi hapa nchini Gifti Stanford maarufu kama ‘Gigy Money’, amewajibu wale wote wanaomwambia kapotea kisanii na kuwaambia kuwa atapambana kuhakikisha anafikia malengo yake.
Akiwapa majibu hayo kupitia kwenye Ukurasa wake wa Instagram Gigy Money amesema, kazi ya usanii haihitaji kuwa na pesa zaidi ya kupata sapoti kutoka kwa watu wako wa karibu kama ilivyokuwa nao yeye.
“Mimi kupendeza si utajiri. Kua msanii akuhitaji pesa kunahitaji supoti na watu wa karibu kama nilio nao mimi, wananishika mkono kila napokwama au kuanguka na kuhakikisha sikati tamaa katika ndoto zangu.Kwa hiyo nyie kuniona mimi napotea bado sana yani labda Mungu aamue, kwani nimebarikiwa mwenzenu,” amesema Gigy Money.
More Stories
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM wakiburudika kusubiri Uzinduzi Ilani ya CCM 2025-2030
Mwanamitindo Millen Magese apewa kibali kuandaa Miss Universe Tanzania 2025
Pacha Milionea waja na truck mpya “Nyumbani”