Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online
KADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Comrade Enock Koola, ambaye ni msomi wa masuala ya Uchumi na Usimamizi wa Miradi, amechukua fomu ya kugombea Ubunge wa Jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro.
Hatua hiyo inaashiria dhamira yake ya kuchangia kikamilifu maendeleo ya wananchi wa Vunjo kupitia nafasi ya uwakilishi bungeni.
Mbali na taaluma yake, Enock Koola pia ni mfanyabiashara na mdau wa maendeleo ya jamii ambaye amekuwa mstari wa mbele katika kushirikiana na jamii katika miradi ya kijamii na kiuchumi.
Kupitia uzoefu na maono yake, anaamini anaweza kuleta mabadiliko chanya na maendeleo endelevu kwa wananchi wa Jimbo la Vunjo.

More Stories
Serikali yaagiza usalama migodini Lindi
Awamu ya kwanza ya uvutaji wa nyaya katika Mradi wa Chalinze -Dodoma wakamilika
EWURA yatangaza bei ya mafuta