Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
RAIS wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, Mei 19 i, 2024 amewasili katika Ofisi za Ubalozi wa Tanzania nchini Austria na kupokelewa na Mwenyeji wake Mhe. Naimi S. H. Aziz, Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Austria na katika Ofisi za Umoja wa Mataifa Vienna.

Dkt. Tulia yupo Vienna nchini Austria, ambapo anatarajia kushiriki Mkutano wa Kimataifa kuhusu Usalama wa Nyuklia (ICONS-2024) utakaofanyika kuanzia kesho tarehe 20-24 Mei, 2024 akiwakilisha IPU kwenye Mkutano huo.

More Stories
Halmashauri Nkasi yapongezwa kwa kupata hati safi
Kutofahamika kwa taasisi za uwezeshaji kiuchumi nchini chanzo Cha umasikini
Sh.400 mil ,kukarabati makazi ya wazee