Na Mwandishi Wetu,Dodomaa
MBUNGE wa Jimbo la Vunjo Dkt Charles Kimei ametajwa kuwa kinara wa kuzungumzia mahitaji ya wananchi kwa kuwa miongoni mwa wabunge vinara wa kusema, kuchangia au kuhoji katika kila kikao cha bunge la 12 linalotarajiwa kuvunjwa mwishoni mwa mwezi Juni mwaka huu.
Kwa mujibu wa tovuti ya Bunge la Tanzania inaonyesha Dk.Kimei amechangia mara 49 na kuuliza maswali 110 yanayohusu jimboni na yanayogusa Taifa kwa ujumla.

Mbunge huyo ni aina ya viongozi wanaoipenda kazi yao na kuguswa ambao wamekuwa wakioonekana katika majimbo yao wakifanya mikutano ya wananchi kutoa mrejesho, kusikiliza na kutatua kero pamoja na ziara za ukaguzi wa miradi ya maendeleo.

More Stories
Rais Mwinyi aipongeza Kampuni ya Yas kushirikiana na ZHC
Raha ya WiFi za bure na mtego kwa taarifa zako za siri
Mke wa Rais wa Finland atembelea Makumbusho ya Taifa