Na Fresha Kinasa, TimesMajira Online, Mara
MGANGA Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara, Dkt. Joachim Eyembe amekuwa wa 55 kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwania nafasi ya Ubunge wa Jimbo la Musoma Mjini.
Dkt. Eyembe amesema, ameamua kuchukua fomu kutokana na msukumo wa Rais Magufuli kuwataka vijana kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi wa mwaka huu katika kuleta maendeleo kwa wananchi.
Amesema, akipata nafasi atahakikisha anatoa mchango wa maendeleo na kutekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi. ili kuungana na Rais Magufuli ambaye amelipaisha Taifa kiuchumi.
More Stories
Wanachi wahimizwa kusajili biashara,majina ya kampuni BRELA
Manispaa ya Shinyanga yaandikisha wanafunzi wa darasa la kwanza kwa 99%
Wananchi wapongeza huduma ya kliniki ya Sheria bila malipo