Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewasili nchini Kenya kuhudhuria Mkutano wa 18 wa Baraza la Mawaziri wanaohusika na mfumo wa pamoja wa umeme kwa nchi za Mashariki ya Afrika (EAPP Council of Ministers) utakaofanyika tarehe 27 na 28 Februari, 2024 jijini Nairobi.
Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA), Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati amepokelewa na viongozi mbalimbali wakiongozwa na Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. Benard Kibesse akiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Nishati wa Kenya, Mhe. Alex Wachira pamoja na Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Stephen Byabato.



More Stories
Rungwe yajenga soko kukuza uchumi kwa wananchi
Waislamu Mwanza wapokea Ramadhani kwa maandamano ya kidini
Kamati ya kudumu ya Bunge ya utawala,katiba na sheria yaridhishwa ujenzi soko Kariakoo