Na Heri Shaaban, TimesMajira Online, Ilala
Diwani wa Viti Maalum Wilayani Ilala Mwl, Beatrice Edward, ametoa mkono wa Pasaka kwa Watoto wa Makundi Maalum , wa Kituo cha Mwana Islamic Fondation .
Akikabidhi msaada huo Diwani Beatrice alisema watoto wa Makundi Maalum sawa na watoto wengine wanaitaji kupewa faraja na jamii .
” Leo naungana na Katibu wa Mkuu wa DIASPORA Tanzania (TDC) GLOBAL kupeleka sadaka kwa ajili ya sikukuu hii ya Pasaka katika kituo cha Mwana Islamic Fondation” alisema Mwl , Beatrice .
![](https://timesmajira.co.tz/wp-content/uploads/2023/04/IMG-20230409-WA0189-576x1024.jpg)
Mwalimu Beatrice alisema misaada hiyo ya CHAKULA waliotoa katika kituo hicho ni mchele,maharage,Tambi,Mkaa ,nyanya ,Vitunguu ,maziwa ya watoto Lactogen ,karoti ,hoho,na mafuta ya kula .
Aliwashukuru wadau mbalimbali ambao wanamshika mkono kwa ajili ya kituo hicho cha Watoto wa Makundi Maalum kutatua kero mbalimbali .
![](https://timesmajira.co.tz/wp-content/uploads/2023/04/IMG-20230409-WA0188-576x1024.jpg)
Aliwataka Wananchi kujenga tabia ya kutembelea katika makundi maalum kula nao chakula au kuwafatiji kwani wao sawa na watu wengine ambao wanaitaji faraja katika Jamii .
More Stories
Wananchi Temeke watakiwa kulinda amani
Dkt.Mpango aagiza mfumo wa NeST utumike kudhibiti ubadhirifu,aipongeza PPRA
Mpogolo ashauri Ilala kutenga bajeti ya mazingira