May 15, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Biteko atembelea banda la NSSF maonesho ya OSHA

 

NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, ARUSHA

MFUKO wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), umewakumbusha wanachama wake kuwa, huduma zote zinazohusiana na uanachama wa mwanachama zinapatikana mtandaoni, (PSSSF Kiganjani).

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Dotto Biteko (wapili kulia), akimsikiliza Meneja Uhusiano na Elimu kwa Wanachama, Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Lulu Mengele alipotembelea banda la Mfuko huo, kwenye Maonesho ya Afya na Usalama Mahali pa Kazi (OSHA), katika uwanja wa General Tyre, Njiro jijini Arusha, Aprili 28, 2024.

NSSF, inashiriki katika maonesho hayo ili kutoa fursa kwa wananchi kuweza kupata taarifa kuhusu shughuli zinazotekelezwa na Mfuko huo. Maonesho ya mwaka huu 2024, yamebeba kauli mbiu isemayo, “Athari za mabadiliko ya tabia nchi katika usalama na afya kazini; Sajili eneo la kazi OSHA katika harakati za kupunguza athari hizo.”

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Dotto Biteko (katikati), akizungumza jambo wakati alipotembelea banda la NSSF, kwenye Maonesho ya Afya na Usalama Mahali pa Kazi (OSHA), katika uwanja wa General Tyre, Njiro jijini Arusha, Aprili 28, 2024. Wengine pichani ni Naibu Waziri wa Nchi Ofisis ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Patrobas Katambi, Mkurugenzi Mkuu, OSHA, Khadija Mwenda (wapili kushoto).

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Paul Makonda (kulia) akizungumza na wafanyakazi wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) wakiongozwa na Meneja wa Mfuko huo mkoani Arusha, Josephat Komba (wakwanza kushoto),  wakati alipotembelea banda la NSSF, kwenye Maonesho ya Afya na Usalama Mahali pa Kazi (OSHA), katika uwanja wa General Tyre, Njiro jijini Arusha, Aprili 27, 2024. NSSF, inashiriki katika maonesho hayo ili kutoa fursa kwa wananchi kuweza kupata taarifa kuhusu shughuli zinazotekelezwa na Mfuko huo. Maonesho ya mwaka huu 2024, yamebeba kauli mbiu isemayo, “Athari za mabadiliko ya tabia nchi katika usalama na afya kazini; Sajili eneo la kazi OSHA katika harakati za kupunguza athari hizo.”