Benki ya NMB imeibuka kinara katika tuzo za mlipa kodi mkubwa zinazotolewa na Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA).
Benki hiyo imeshinda tuzo tatu zinazoitambua kama mlipa Kodi Mkubwa nchini kwa mwaka 2021/2022.
Tuzo hizo ni:
1️⃣ Mshindi wa Kwanza; Taasisi inayozingatia misingi na kanuni bora za ulipaji kodi.
2️⃣ Mshindi wa Kwanza; Mlipa kodi mkubwa zaidi katika kundi la taasisi za fedha nchini.
3️⃣ Mshindi wa Tatu; Taasisi inayolipa kodi kubwa zaidi nchini (sekta zote).
Mafanikio haya ni matokeo ya benki hiyo kuzingatia kanuni bora za ulipaji kodi, ufanisi katika kujiendesha na ubunifu wa suluhishi bora za kifedha zenye manufaa kwa wateja.
Benki ya NMB imedhamiria kuendelea kuendesha biashara yake kwa kuzingatia sheria na kanuni za nchi ili kuchangia kikamilifu ujenzi wa uchumi wa Taifa.


More Stories
Kihenzile ahamasisha uwekezaji sekta ya anga
Wafanyabiashara watuliza wananchi hofu ya bei ya bidhaa
TISEZA kuanzisha madawati ya uwekezaji kila Halmashauri za Wilaya