Na Judith Ferdinand,TimesMajira Online, Mwanza
JESHI la Polisi Mkoa wa Mwanza linamsaka baba mzazi, Adam Athuman (30-40) kwa tuhuma za za kumuua mtoto wake huko katika Kata ya Buswelu Wilaya ya Ilemela Mkoa wa Mwanza.
Tukio hilo lilitokea Novemba 22, 2020 majira ya saa 5:30 huko Kata ya Buswelu wilayani Ilemela mkoani Mwanza.
Akizungumza mkoani hapa, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, ACP Muliro Jumanne amesema, marehemu huyo ambaye jina lake ni Athuman Adam mwenye umri wa miaka 10 aliyekuwa mwanafunzi wa darasa la tatu shule ya msingi Nyamadoke Kata ya Buswelu Wilaya ya Ilemela,aliuawa kwa kile kilichodaiwa kushambuliwa na fimbo sehemu za mwili wake.
More Stories
Rungwe yajenga soko kukuza uchumi kwa wananchi
Waislamu Mwanza wapokea Ramadhani kwa maandamano ya kidini
Kamati ya kudumu ya Bunge ya utawala,katiba na sheria yaridhishwa ujenzi soko Kariakoo