Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online
MSANII wa muziki wa staili ya miduara kutoka Zanzibar
AT, amemshukuru msanii wa muziki wa Bongo fleva na Bosi
wa Kondegang Rajabu Abdul maarufu kama ‘Harmonize’ kwa
kumfanya aonekani kwenye ramani ya mziki kwa sasa.
Akitoa shukrani hizo, AT amesema Harmonize ni kijana
pekee mwenye uthubutu wa kumsaidia kila mtu, kwani
amekuwa naye karibu na kufanya naye mambo makubwa.
“Nimekuwa nikifanya kazi kwa Kuzingatia Ukubwa wako na
Heshima ya Watu wetu wote. Nichukue nafasi hii
kukushukuru wewe Harmonize na kila shabiki wako na
Uwongozi Mzima Kwa kufanya Leo AT azungumzike,
atizamike Upya, pamoja na kuwashukuru kwa Dhati Media’s
Zote kwa kila sekta na Fans wangu na Wasanii wenzangu
wote wanaonipenda na wasionipenda mimi niseme Shukran
sana sana Mubarikiwe.
Naomba nitoe ahadi ya kufanya Kazi nzuri zaidi na kwa
uadilifu. Wazanzibar naomba niwaambie tu. Huyu Kijana
ni ndugu yetu, anaroho ya kipekee tokea nimekuwa nae
karibu na Kuna Makubwa kwa Bara na Visiwani kwetu. Kaa
tayari kupata kitu kizuri,” amesema AT.
More Stories
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM wakiburudika kusubiri Uzinduzi Ilani ya CCM 2025-2030
Mwanamitindo Millen Magese apewa kibali kuandaa Miss Universe Tanzania 2025
Pacha Milionea waja na truck mpya “Nyumbani”