Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online
MSANII wa rap nchini Marekani A$AP Rocky, amefunguka kuhusu mahusiano yake na mpenzi wake Rihanna na kusema anajiona mtu mwenye bahari ya kubarikiwa na Mwenyezi Mungu kuwa na mpenzi kama Rihanna.
Akizungumzia hilo, A$AP Rocky amesema Rihanna amekuwa msaada mkubwa sana kwenye maisha yake kwani alikuwa bega kwa bega wakati anatambulisha makala yake ya Stockholm Syndrome iliyohusu stori yake ya kukamatwa na kutiwa jela nchini Sweden mwaka 2019.
“Nilitaka tu kusimulia stori yangu bila kuonekana na lalamika au nimeonewa”. Kwenye makala hiyo A$AP Rocky anasimulia tukio la mwaka 2019 jinsi timu yake ilivyogombana na vijana wawili huko nchini Sweden na kujikuta akiwekwa jela bila dhamana sababu alikuwa mgeni.
More Stories
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM wakiburudika kusubiri Uzinduzi Ilani ya CCM 2025-2030
Mwanamitindo Millen Magese apewa kibali kuandaa Miss Universe Tanzania 2025
Pacha Milionea waja na truck mpya “Nyumbani”