September 27, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Access Bank yakidhi vigezo vya kisheria katika ununuzi wa BancABC Tanzania

Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online

Access Bank PLC imekamilisha mchakato na kukidhi vigezo vyotevya kisheria na vya kikanuni kuhusiana naununuzi wa African Banking CorporationTanzania Limited (BancABC Tanzania). Sasa taasisi hii inaitwa Access Bank Tanzania Limited, jambo ambalo linapanua zaidi uwepowa Access Bank katika ukanda wa Afrika Mashariki.


Hatua hii itakuwa ni mwendelezo uliofuatana naununuzi wa wateja binafsi, na wafanyabiasharawa kati wa Standard Chartered Bank Tanzania. Taasisi hii mpya ya Access Bank Tanzaniaitatumia uzoefu wake pamoja na ule wakampuni yake mama – Access Bank ili kutoamasuluhisho mapana ya kibenki kwa lengo la kuendeleza ukuaji wa kiuchumi nchini Tanzania.

Akizungumzia hatua hii muhimu, Seyi Kumapayi, Mkurugenzi Mtendaji wa matawi yaAccess Bank barani Africa alisema:
“Hatua hii ni hatua muhimu sana katika mkakatiwetu wa ukuaji Afrika Mashariki, ikithibitishadhamira yetu ya kuchangia maendeleo yakiuchumi nchini Tanzania. Kwa kuunganishaBancABC Tanzania katika kundi la Access Bank, tutaongeza uwezo wetu wa kutoamasuluhisho mbalimbali ya kifedhazinazobuniwa kukidhi mahitaji ya wateja wetuyanayobadilika kulingana na kasi ya ukuaji wauchumi, lengo letu ni kuwezesha biashara zaidikati ya nchi za Africa, huku tukiendelea kuinuajamii kwa kulenga hasa wanawake na vijana, kupitia huduma bora za kibenki na fursa za kifedha.”

John Imani, Mkurugenzi Mtendaji wa Access Bank Tanzania, pia alitoa maoni yake akisema,“Tunafuraha kubwa kuwa sehemu rasmi yafamilia ya Access Bank. Hatua hii inafunguafursa mpya kutokana na ubobefu wa taasisizote mbili zinazounda benki imara zaidi nayenye ushindani wa hali ya juu utakayokidhimahitaji ya wateja wetu. Tunaahidi kuendeleakutoa huduma bora huku tukikua pamoja nchiniTanzania.”

Ununuzi huu utawanufaisha wateja wa Access Bank Tanzania kwa kuwa na huduma zenyekiwango cha kimataifa, na mfumo wa kipekeewenye ushirikiano wa kimataifa. Zaidi ya hayo, uwepo wa Access Bank unaimarisha biasharabarani Africa kwa kujenga daraja la miamala yakibenki ndani na ya nje ya nchi kwa ufanisi zaidikwa kuleta suluhisho za kisasa kwa kutumiaushirikiano wake na wadau wake wa kimataifa.

Benki hii inaahidi kuendelea kujitoa kwakuweka rekodi yake ya mafanikio katikakusaidia jamii na kuhifadhi mazingira kwenyeoperesheni zake za kibenki katika mataifambalimbali ambako ipo, hii inaashiria ni kwanamna gani Benki hii imejipanga kuletamaendeleo ya kiuchumi pamoja na kutunzamazingira na maendeleo ya jamii kwa ujumla. Kupitia juhudi hizi, Access Bank Tanzania itachangia kuunda mustakabali endelevu zaidikwa taifa.