March 7, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

CCM kuhuisha mchakato wa Katiba mpya

Na Agnes Alcardo, Timesmajira Online-Simiyu

MGOMBEA Mwenza wa nafasi ya Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amesema, katika kipindi cha miaka mitano ijayo endapo chama hicho kitashinda katika uchaguzi mkuu kitahuisha mchakato wa Katiba mpya.

Dkt.Nchimbi ametoa kauli hiyo Septemba Mosi 2025,Kata ya Dutwa mkoani Simiyu, ikiwa muendelezo wa kampeni ya chama hicho kwa ajili ya kuomba kura kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 29,2025.

Amesema sambamba na mpango huo CCM imedhamiria ndani ya miaka mitano ijayo itaendelea kusimamia na kudumisha amani kwa Watanzania.