March 7, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

MOI yatii agizo la Rais kuendela kutoa huduma Nanenane hadi Agosti 10,2025

Na Mwandishi Wetu,Dodoma

Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo na Muhimbili (MOI) imetii agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan la kuendelea kutoa huduma za kibingwa na kibobezi kwenye Maonesho ya Nanenane, Viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma, hadi Agosti 10, 2025.

Awali, huduma hizo zilipangwa kuhitimishwa tarehe 8 Agosti 2025, lakini kufuatia agizo la Rais, MOI itaendelea kuhudumia wananchi kwa siku mbili zaidi ili kuhakikisha watu wengi zaidi wananufaika na huduma hizo muhimu