March 7, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Enock Koola achukua fomu ya kugombea ubunge Vunjo

Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online

KADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Comrade Enock Koola, ambaye ni msomi wa masuala ya Uchumi na Usimamizi wa Miradi, amechukua fomu ya kugombea Ubunge wa Jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro.

Hatua hiyo inaashiria dhamira yake ya kuchangia kikamilifu maendeleo ya wananchi wa Vunjo kupitia nafasi ya uwakilishi bungeni.

Mbali na taaluma yake, Enock Koola pia ni mfanyabiashara na mdau wa maendeleo ya jamii ambaye amekuwa mstari wa mbele katika kushirikiana na jamii katika miradi ya kijamii na kiuchumi.

Kupitia uzoefu na maono yake, anaamini anaweza kuleta mabadiliko chanya na maendeleo endelevu kwa wananchi wa Jimbo la Vunjo.