Na Esther Macha, TimesMajira Online, Mbeya
BAADHI ya wagonjwa na baadhi ya mali katika Hospitali ya Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya wamenusurika na kuungua moto baada ya majengo mawili ambayo ni wodi ya watoto na wazazi kuwaka moto leo mchana, huku chanzo cha moto huo kikiwa bado hakijajulikana.
Akizungumza na TimesMajira wakati akiwa katika eneo la tukio Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Claudia Kitta amesema wamefanikiwa kuokoa wagonjwa na baadhi ya samani na vifaa tiba vya hospitali hiyo.
“bado chanzo cha moto hakijafahamika na japo tumefanikiwa kuokoa wagonjwa, na baadhi ya samani na vifaa tiba vya hospitali hiyo.” Amesema Mkuu wa Wilaya Claudia Kitta
More Stories
Mbunge ahoji ukamilishwaji miundombinu Vituo vya afya
Mbogo aomba Tume kuchunguza madai ya waliokuwa wafanyakazi wa EAC
Dkt.Mabula aomba mabonde Ilemela yatumike kwa Kilimo cha umwagiliaji