Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online
TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imesema zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya pili mzunguko wa pili ulioanza Mei 16 hadi 22, 2025 ukikamilika Tume haitaongeza siku za ziada.
Tume hiyo imesema, wananchi wenye sifa wajitokeze katika siku mbili zilizobaki kujiandikisha au kuboresha taarifa zao na kuwaondoa wale wasio na sifa kuwepo kwenye Daftari hilo.
Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa Tume, Jaji wa Rufani, Jacobs Mwambegele wakati wa ziara ya kukagua mwendendo wa zoezi hilo la Uboreshaji na uwekaji wazi Daftari la Awali katika Halmashauri za Wilaya ya Lushoto Mkoani Tanga, yenye majimbo ya Uchaguzi ya Lushoto na Mlalo.

Kwa upande wake Afisa Mwandikishaji Jimbo la Lushoto na Mlalo, Dkt. Ikupa Harrison Mwasyoge ameeleza namna uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na Uwekaji Wazi wa Daftari la Awali unavyoendelea.
Zoezi hilo linakwenda sambamba na uwekaji wazi wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura katika mikoa 11 ya Tanzania Bara na Mitano ya Tanzania Zanzibar.
Mikoa hiyo ni Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Tanga, Morogoro, Pwani, Singida, Dodoma, Dar es Salaam, Lindi, Mtwara, Mjini Magharibi, Kaskazini Unguja.
Kusini Unguja, Kaskazini Pemba na Kusini Pemba ambapo zoezi hilo linafanyika kwa siku saba na lilianza Mei 16 hadi 22, 2025.
Katika zoezi hilo vituo vinafunguliwa Saa 2:00 asubuhi na kufungwa Saa 12:00 jioni kila siku kwa siku saba na kauli mbiu ya zoezi ni “Kujiandikisha kuwa mpiga kura ni msingi wa uchaguzi bora’.

More Stories
WMA wawataka watoa huduma kuzingatia uwiano sahihi
Bodi ya ETDCO yaridhishwa na maendeleo ya mradi wa umeme Tabora
Dkt.Biteko mgeni rasmi maadhimisho miaka 35 ya TAWLA