Na Heri Shaaban, Timesmajira Online,Ilala
DIWANI wa Kata ya Ilala Saady Khimji,amesema atamlipia gharama za fomu kwa nafasi ya Ubunge katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025,Mbunge wa sasa wa Jimbo la Ilala Mussa Zungu.
Kimji ,amesema hayo wakati wa kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi(CCM),ambapo ameeleza sababu ya kufanya hivyo ni kuwa Ilala bado inamhitaji Mbunge huyo.
Amesema awali alikabidhi kiasi cha milioni 1,kwa ajili ya kumchangia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan, kugombea Urais katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka huu.
More Stories
Mke wa Rais wa Msumbiji,Gueta atembelea JKCI
Kadinali Robert Prevost achaguliwa kuwa Papa Leo wa XIV
Viongozi wa Dini waaswa kuimarisha mafundisho kwa wanandoa kunusuru kuvunjika kwa ndoa